Translate

Mourinho: Tulidhibiti mechi na kuwanyamazisha mashabiki wao


Mkufunzi wa man United Jose Mourinho

Mkufunzi wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amesema kuwa timu yake ilidhibiti mpira pamoja na kufunga midomo ya mashabiki wa Anfield.

Akihojiwa baada ya mechi hiyo iliotoka sare ya bila kwa bila,Mourinho amesema kuwa ijapokuwa hakutarajia matokeo hayo timu yake ilifanikiwa kuizuia Liverpool kwa kudhibiti mchezo kwa muda mrefu.

''Tulifanikiwa kudhibiti kelele za mashabiki wa Anfield pamoja na mchezo wa timu yao''.

Mourinho amesema kuwa ijapokuwa wengi walidhani watashindwa timu yake iliodhibiti mpira na kuwapatia kibarua kigumu wapinzani wao.

Hatahivyo mkufunzi huyo amekiri kwamba safu ya ushambuliaji ya Manchester United haikuwa imara wakati wa mechi hiyo.

''Hatahivyo nadhani hatukuimarika vilivyo katika safu ya mbele.Nashukuru kwamba pointi yetu moja iliwazuia kupata tatu''.

Aliongezea kwamba timu yake ina kibarua kigumu katika uwanja wa Stamford bridge wikendi ijayo na hivyobasi watalazimika kuimarika.

Katika mechi hiyo Liverpool lifanikiwa kudhibiti mechi kwa asilimia 65 huku Manchester United ikidhibiti asilimia 35.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment